Sunday, December 20, 2015

Heshima kwa Kina mama wote..

 
Nilikuwa nawadharau sana wanawake niliwaona kama viumbe dhaifu wasio na akili na hii ilitokana na mazingira niliyokulia ambapo mwanamke anadharaulika na kubezwa.
Wiki iliyopita nilimpeleka mke wa kujifungua kwenye hospitali ya private ambapo hospitali hiyo ina utaratibu wa kumzalisha mwanamke mmewe wake akiwa pembeni anaangalia, aisee kuzaa ni shughuli asikwambie mtu nilitoka labour nduki mpaka sasa nikifikria kitendo kile nimeanza kuwaheshimu wanawake .
Kama hospitali zote zingelikuwa na utaratibu ule hakika wanaume tungewaheshimu wake zetu, mama zetu na wanawake wote kwa ujumla acha mama aitwe mama.

Credit to JamiiForums.com